Monday, October 23, 2017

Semina ya Kuongeza Uelewa juu ya Ualbino na Kupinga mauaji ya watu wenye Ualbino yafanyika wilayani Bukombe.

Mwenyekiti wa Chama cha watu wenye UALBINO Tanzania  (TAS- BUKOMBE) Bi.Ida Saka amekemea vikali mauaji yanayoendelea kwa watu wenye ualbino Tanzania.
 Amesema hayo kwenye warsha ya Mradi Jumuishi wa watu wenye ualbino iliyofanyika wilayani Bukombe ikishirikisha wadau mbalimbali yakiwemo madhehebu ya dini,waganga wa jadi,watumishi wa serikali huku Mgeni Rasmi akiwa Mkuu wa wilaya ya Bukombe aliyewakilishwa na Ndugu Ally Mketo Afisa Tawala wa Wilaya.


Mwenyekiti wa Chama cha  watu wenye Ualbino Bukombe Bi.Ida Saka.
Mgeni Rasmi aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Bukombe ambaye ni Afisa Tawala Ndugu Ally Mketo.
 Amesema “Watu wenye Ualbino wana haki sawa kama wanadamu wengine na wana uwezo wa kusoma,kufanya kazi,kuishi inashangaza sana kuona vitendo vya kikatili vinafanywa na watu ambao mimi nasema hawana Hofu ya Mungu, Mimi kwetu Babu yangu ni Albino lakini mbona mimi mjukuu wake si Albino,Ndugu zangu elimu tutakayo pata hapa tuifikishe na kwa wengine ili ukatili ukome kbsa.
Mratibu wa Mradi Jumuishi wa watt wenye Ualbino wilaya ya Bukombe Ndugu Emmanuel Simon.
Mwezeshaji wa Mradi Jumuishi wa watu wenye Ualbino ambaye pia ni Mwalimu wa Somo la Biology katika Shule ya Sekondari Runzewe Ndugu  Simon Mashauri   akitoa maswali kwa vikundi baada ya kufundisha nini Maana ya  Neno “Albino”, mtu anakuaje Albino,Haki za watu wenye Ualbino,Sheria ya Makosa ya Jinai na Sheria ya watu wenye Ulemavu ya  No.9 ya mwaka 2010.
Mtoto Hamad nae alikuja kwenye semina na Mama yake Bi.Halima .


Mganga wa Jadi Bi.Sada akiwa akisema Jambo wakati wa semina  ya mradi jumuishi  wa watu wenye Ualbino.

Afisa Mipango wa Wilaya Bi.Sarah Yohana na Afisa Maendeleo ya Jamii Bi.Prisca Lyimo wakisikiliza semina ya Mradi Jumuishi wa watu wenye Ualbino.

Viongozi wa Kidini Kutoka Madhehebu mbalimbali nao wakisikiliza Semina Jumuishi katika Ukumbi wa Halmashauri.
Diwani wa Kata ya Katente Mhe.Bahati Kayagila akichangia mada katika semina ya Mradi Jumuishi wa watu wenye Ualbino amesema “Watu wenye Ualbino wana haki zote sawa na watu wasiokuwa na ualbino ni muda sasa wa kuendelea kupambana na watu wakatili  kila mmoja atoke humu na kusambaza elimu hii na tukawe wa fuatiliaji wa matukio haya ya kikatili” amesisitiza
Kazi za Vikundi baada ya Kupewa maswali na muwezeshaji.
Bi. Eliwaje Wa Dawati  la Jinsia wilaya ya Bukombe.


Kazi ya Vikundi ikiendelea ambapo vikundi vine kwa awamu mbili zilijibu maswali ya mwezeshaji na kuwasilisha.

No comments:

Post a Comment