Friday, October 27, 2017

Asali yaing'arisha Bukombe Maadhimisho ya Chakula Duniani Mkoani Geita.


Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Taifa (FAO) na Shirika la Mpango wa Chakul duniani (WFP) yavutiwa sana na zao la Nyuki (Asali) pamoja na zao la Muhogo kutoka wilaya ya Bukombe katika maonyesho ya siku ya Chakula yaliyofanyika Mkoani Geita.
Na hivyo kuamua kutembelea wilaya ya Bukombe kujionea Uzalishaji wa mazao hayo katika uhalisia wake ili kutimiza dhana ya Uanzishwaji wa Viwanda kwa kukaribisha wawekezaji.  
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Mhe.Josephat Maganga akiongea na wageni waliofika Ofisini kwake kutokea Shirika la  Mpango wa Chakula Duniani (WFP) na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Taifa (FAO)pamoja na The International Institute of Tropical Agriculture (IITA).

Mwakilishi Mkazi kutoka Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) Bi. Neema Sitta katika Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Bukombe.

Mwakilishi Mkazi kutoka Shirika la Chakula na Kilimo Umoja wa Taifa (FAO) Bwana. Fred Kaferelo katika Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Bukombe.

Dr Fred Baijyuka kutoka kutoka The International Institute of Tropical Agriculture (IITA)  akijitambulisha alipofika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bukombe kwa lengo la kuona Soko la Zao la Muhogo wilayani hapa.


Katika ziara hii ya wageni kutoka Mashirika ya Chakula walifika na kutaka kujionea uhalisia wa uzalishaji wa zao la Nyuki yani Asali na Nta.
Kwa mwaka jana vikundi mbalimbali vya uzalishaji Asali wilayani hapa viliweza kuzalisha Tani 300. Mwaka huu  kuanzia mwezi wa 7 mpaka sasa tani 237 zimesafirishwa nje ya nchi na Tani 76 zimesafirishwa ndani ya Nchi. Pamoja na zoa linguine la Nyuki Yani Nta Tani 22 imesafirishwa  ndani ya nchi.

Hizi ni Asali ambazo zipo kwenye Vifungashio tayari kwaajili ya kuuzwa madukani,sokoni. Asali inayoonekana Nyesui sana ni Nyuki wadogo na sali inayoonekana sio Nyeusi ni Nyuki wakubwa.
Afisa Nyuki wilaya ya Bi.Dafroza Shayo akifafanua uzalishaji  wa zao la Nyuki (Asali) kwa wageni kutoka mashirika mbalimbali yanayohusiana na Chakula na Kilimo wilayani Bukombe.
Mzalishaji wa Asali kutoka kijiji cha Msonga kata ya Runzewe Mashariki Bwn. Obadiah akizungumza namna anavyozalisha zao hili la Nyuki.
Baadhi ya Madumu yaliyojaa Asali.
Madumu na Ndoo lita 20 zilizojaa Asali kwaajili ya kuanza kuchunjwa.

Hapa ndipo Asali inapochunjiwa ili kuweza kwenda hatua nyingne ya mwisho ya kuchuja na tayari kuwekwa kwa vifu,ngashio.


Vipaumbele vya Halmashuri ya wilaya ya Bukombe ni kuendelea kuibua miradi ya maendeleo kwaajili ya maendeleo ya wilaya. Mradi wa Soko la Mihogo ni kwa maendeleo ya wana Bukombe wanaolima sana zao la Muhogo ambalo limekuwa likihitajika sana katika nchi za jirani Uganda,Rwanda,Burundi na Demokrasia ya Kongo.
Afisa Kilimo Bwn.Joseph Machibya akielezea mradi wa Soko la Mihogo lililopo kata ya Namonge wilayani hapa kwa wageni waliofika kulitembelea.

Hili ndilo Soko la Kimataifa la zao la Muhogo lilipo kata ya Namonge wilayani Bukombe ambalo lilipata nafasi ya kutembelewa na wageni kutoka Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Taifa (FAO) ,Shirika la Mpango wa Chakula Duniani(WFP) na The International Institute of Tropical Agriculture (IITA) ili kuona fursa za Uwekezaji katika uanzishaji wa Viwanda wilayani hapa. 
Sehemu ya Kuweka Macao kwa wafanyabiashara wa Soko hili.
Meza za  kuwekea zilizojengwa katika Soko hili.
Hili ndilo Jengo la kuwekea mazao kwaajili ya kuuza nan je halo ni kichujio cha zao la Muhogo Baada ya Kuoshwa ili maji yakauke.

                               Maghala ya Kuhifadhia Mazao katika Soko la Mihogo .

No comments:

Post a Comment