Bukombe
imekuwa katika jitihada za kuendelea kuboresha utoaji huduma kwa jamii katika
sekta mbalimbali ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na kutekeleza
mipango ya bajeti.
Kwa
mujibu wa takwimu zilizotolewa hivi karibuni na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa
na Serikali za Mitaa, Halmashauri ya wilaya ya Bukombe imekuwa ya Pili kwa Mkoa wa Geita katika Utoaji
huduma bora kwa wananchi kwa kuzingatia Sera,Kanuni, na viwango vilivyowekwa
kwa kila sekta ya huduma za jamii hususani katika sekta za Afya,Maji,Elimu,Barabara na Usimamizi wa
Fedha.
Takwimu
hizi zimejikita katika matumizi sahihi ya fedha kwa ujumla kwa kutumia taarifa
za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) ya Mwaka 2015/2016
pamoja na taarifa ya kamati ya Hesabu za serikali za Mitaa.
Katika
mchanganuo huo Halmashauri ya wilaya ya Bukombe imeshika nafasi ya pili
katika Mkoa wa Geita kwa jumla ya alama 60.83 ikitofautiana kwa alama 11.94 tu na Halmashauri iliyoongoza
Kitaifa yenye jumla ya alama 72.73.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Bukombe anapenda kuwashukuru wananchi wote
ambao ndiyo wadau wakubwa wa maendeleo wilayani hapa katika kufanikisha utekelezaji makini wa
shughuli zote za kila siku.
Aidha
changamoto hazikosekani hivyo tunaahidi kuboresha huduma bora na za kisasa kwa
kushirikiana na wananchi ili kuhakikisha tunazipunguza kama si kumaliza kabisa
changamoto zinazojitokeza kwa sekta zote kwa maelekezo ya serikali ya awamu ya
tano.
TUSHIRIKIANE
WANA BUKOMBE 2017.
IMETOLEWA NA;
KITENGO CHA TEKNOLOJIA, HABARI NA MAWASILIANO.
BUKOMBE
8/11/2017
No comments:
Post a Comment